Gundua tofauti kati ya bondi, hisa, na mifuko ya pamoja kwa uharaka na urahisi ili uanze kuwekeza leo.
Umesikia kuhusu uwekezaji, au
Umesikia watu wakiongelea bondi, hisa, na mifuko ya pamoja,…
lakini haujajua tofauti zao na wapi pa kuanzia kuwekeza.
Kama huyu ni wewe, katika ujumbe huu utagundua tofauti 12 muhimu, na utaweza kuchagua kwa urahisi wapi pa kuanzia.
Tukianza na kuwekeza,…
Ni kutumia fedha uliyokusanya au kuweka akiba ili kuzalisha fedha nyingine au faida.
Haya sasa, swali la kwanza la msingi;
Hisa, Bondi, na Mfuko wa Pamoja wa Uwekezaji ni nini?
Hisa ni umiliki wa sehemu ya kampuni au biashara. Kwa kiingereza inajulikana kama stock.
Hisa huuzwa kwa idadi na kwa bei ya kampuni husika yaani, stock price.
Mfano wa makampuni ya kitanzania yanayouza hisa ni Benki ya CRDB, Benki ya NMB, na Tanzania Portland Cement (Twiga Cement -TPCC).
Bondi ni uwekezaji ambao unaikopesha serikali au taasisi ili upate riba katika kipindi cha muda fulani.
Serikali, taasisi au kampuni inazitumia fedha hizo ili kuzalisha faida, na mwekezaji hurejesha anarudishiwa pesa yake baada ya muda wa bondi hio kuisha.
Bondi zinazotolewa na serikali zinaratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ‘Treasury Bonds’, na kuna bondi za;
✔ Manispaa ‘Municipal Bonds’,
✔ Makampuni ‘Corporate Bonds’, na za
✔ Kimataifa ‘International Bonds’.
Mfuko ya Pamoja ya Uwekezaji ni mfuko ambao watu wengi huwekeza pesa zao na huwa unasimamiwa na wataalamu wa fedha.
Baada ya taasisi husika kukusanya fedha hizo, wanawekeza katika Soko la Fedha ili kuzalisha faida ambayo baadae hugawanywa kwa wawekezaji.
Mifuko ya namna hii huwa inaahidi ongezeko la pesa yako mpaka asilimia 12% kwa mwaka…
ingawa hautakiwi kusahau ya kwamba kila uwekezaji una hatari / ‘risk’ ya kupoteza pesa.
Mfano wa mifuko hii ni kama,
✔ Mfuko ya Umoja (UTT Amis)
✔ Mfuko wa Watoto (UTT Amis)
✔ Mfuko wa Bond (UTT Amis)
✔ Mfuko wa Ukwasi (UTT Amis)
✔ Mfuko wa Faida
✔ M-Wekeza, na
✔ Mfuko wa Sanlam Pesa
Tofauti kati ya Hisa, Bondi, na Mfuko wa Pamoja wa Uwekezaji
| HISA | BONDI | MIFUKO YA PAMOJA | |
| MAANA | Umiliki wa sehemu ya Kampuni | Kuikopesha serikali au taasisi | Wawekezaji wengi kwenye mfuko mmoja |
| ZINAUZWA KAMA (UNITS)… | Hisa Moja, kulingana na kampuni | Bondi Moja, shilingi 100/= | Kipande Kimoja (Net Asset Value per Unit) |
| FAIDA | Gawio (Dividend)Kukuza Mtaji (Capital Growth) | Riba (Interest)Kukuza Mtaji; inategemea na bei utakayonunulia au kuuza | 1. Gawio (Dividend)2. Kukuza Mtaji (Capital Growth)) |
| KIWANGO CHA FAIDA | Kiwango kinategemea na maendeleo ya kampuni ulilochagua | Kuanzia 8.5% kwa bondi za miaka mitatu na kuendelea | Ahadi ya mpaka 12% kwa mwaka |
| KIWANGO CHA CHINI CHA KUANZIA | Bei ya Hisa 10 ya kampuni utakalochagua | Kuanzia 500,000/= mpaka 1,000,000/= (inategemea aina ya bondi) | Kuanzia 10,000/= kutokana na mfuko uliochagua |
| MUDA WA UWEKEZAJI | Endelevu | Miaka kutokana na bondi husika | Endelevu au Miaka kutokana na mfuko husika |
| URAHISI WA KUIPATA PESA (LIQUIDITY) | Utaweza kuuza pakiwa na wanunuaji sokoni | Unaweza ukauza siku 2 za kazi baada ya manunuzi kukamilika | Inaongoza kwa urahisi, kutokana na mfuko uliochagua |
| HATARI YA KUPOTEZA | Kubwa Zaidi | Ndogo Zaidi | Wastani |
| UWEZEKAJI MCHANGANYIKO (DIVERSIFICATION) | Uwekezaji ni hisa peke yake | Uwekezaji ni bondi uliyonunua | Unaweza ukawa kwenye rasilimali tofauti kama hisa, bondi, na call accounts |
| GHARAMA | Mauzo na manunuzi huwa na makato ya kodi, ‘broker’/wakala, na taasisi za uwekezaji | Makato ya kodi kwenye faida hayapo kwa bondi zaidi ya miaka miwili | Makato yanategemeana na mfuko |
| USIMAMIZI WA KITAALAMU | Wewe unafanya maamuzi ya uwekezaji | Wewe unafanya maamuzi ya uwekezaji | Wataalamu wa uwekezaji wanafanya maamuzi |
| USHAURI NA ELIMU KABLA YA KUWEKEZA | Inahitajika kwa kiwango kikubwa | Ni muhimu | Ni muhimu |
Baada ya kujua haya, unaweza kuchagua ni uwekezaji upi unaanza nao, kama ni Bondi, Hisa, au Mifuko ya Pamoja ya Uwekezaji.
Na,
unaweza ukapakua (download) tracker hapa chini kwa ajili ya urahisi wa kufuatilia uwekezaji wako kila mwezi:

Usiache kufuatilia ukurasa wa Instagram kupata free content, na bofya kitufe hapo chini kuwasiliana nasi WhatsApp.
PS:
Malengo yako kwa kiasi kikubwa ndio yanakurahisishia safari yako ya uhuru wa kifedha.
Anza leo!
Kila la kheri.
Wako katika pesa,
Gracing Money!
Marejeo:
1] UTT-AMIS, uttamis.co.tz
2] Dar-es-Salaam Stock Exchange, dse.co.tz
3] Bank of Tanzania, bot.go.tz
4] Watumishi Housing Investment, whi.go.tz
5] M-Wekeza, vodacom.co.tz6] Sanlam Pesa Money Market Fund, invest-tz.sanlameastafrica.com
Follow us on Socials

Read More Blog Posts
Umesikia Kuhusu Mifuko Sita (6) ya Uwekezaji ya iTrust?
Mifuko ya Uwekezaji ni mingi…na itazidi kuongezeka Je, umesikia kuhusu Mifuko ya Uwekezaji ya Pamoja… Imeongezeka na itaendelea kuongezeka. Kwa sasa ipo…
UTT ni nini?
UTT ni njia rahisi ya kuwekeza kwa watanzania. Elewa inavyofanya kazi na jinsi ya kuanza kuwekeza. Inawezekana umesikia kuhusu UTT lakini…
Jinsi ya Kuingia Kwenye Soko la Fedha BILA KWENDA KINYUME
Mwongozo wa Muislamu Kushiriki Soko la Fedha kwa Njia Halali na ya Kiimani Umesikia watu wanaongea kuhusu uwekezaji, kila kona ya…
Je, Wewe Kuwekeza Kwenye Kampuni la NICOL Utakua ni Uamuzi
Je, Wewe Kuwekeza Kwenye Kampuni la NICOL Utakua ni Uamuzi Sahihi? Kwenye picha hapo juu ni swali zuri nimeshawahi kuulizwa, na lilikua…
Jinsi ya Kuendesha Biashara Yako BILA KUPOTEZA UHURU Wako wa
Soma mpaka mwisho kama, una biashara ya kutoa huduma (service based business) au kuuza bidhaa (brick-and-mortar business), lakini unakabiliana na changamoto hizi; ✔…
VITABU VITANO Vinavyoweza KubadilishaMtazamo WAKO Kuhusu Pesa YAKO
Unataka kubadilisha mtazamo wa uchumi wako? Vitabu hivi vitano (5) vinaweza kubadilisha unavyofikiri kuhusu kipato, akiba na kukuza pesa yako. 6…
