UTT ni njia rahisi ya kuwekeza kwa watanzania. Elewa inavyofanya kazi na jinsi ya kuanza kuwekeza.
Inawezekana umesikia kuhusu UTT lakini hujajua watu wanaongelea nini…
Au unajua kwamba ni UTT ina mifuko tofauti lakini hujajua hio mifuko ni kwa ajili gani.
Utakaposoma mpaka mwisho, utaweza kuelewa UTT ni nini hasa, na mifuko yake ina tofauti ipi,
tukianza na uwekezaji…
Kuwekeza ni kutumia fedha uliyokusanya au kuweka akiba ili kuzalisha fedha nyingine au faida.
Njia mojawapo ya kuwekeza ni kukusanya fedha pamoja na wawekezaji wengine halafu kugawana faida, hii ndo inaitwa Mifuko ya Pamoja ya Uwekezaji,
na UTT-AMIS (Unit Trust of Tanzania – Asset Management and Investor Services),
ni taasisi mama ya uwekezaji wa pamoja hapa kwetu Tanzania, ilioanzishwa mwaka 2003.
UTT inamilikiwa na serikali, chini ya Wizara ya Fedha.
UTT inafanyaje kazi?
Pesa za wawekezaji zinapokusanywa, zinawekezwa kwenye rasilimali nyingine za fedha kama Bondi, Hisa na Akaunti za Akiba za Muda Mfupi (Call Accounts).
Uwekezaji wa fedha hizi unafanywa na wataalamu wa uwekezaji, na
..hii ni faida kubwa mojawapo ya kuwekeza kwenye mifuko ya pamoja.
Hatifungani (Bondi) mara nyingi huwa na kianzio cha 1,000,000/= na unapowekeza katika Hisa, inahitaji wewe mwenyewe kufuatilia.
Sio kila mtu anaweza kuwa na 1,000,000/= ya kuwekeza na sio kila mtu ana muda na utaalamu wa kufuatilia hisa,…
kwahio mifuko ya uwekezaji unasaidia watu wa hali zote kuweza kuwekeza.
Mifuko ya UTT inakuahidi ongezeko la pesa yako kwa angalau asilimia 12% kwa mwaka au angalau 1% kwa mwezi.
Mfano;
Unapowekeza au kuweka akiba ya 100,000/= leo, ndani ya mwaka hela inaweza ikakua mpaka 112,000/=
Lakini pia ni vizuri kujua,
Uwekezaji wowote lazima uje na hatari ya kupoteza (risk) ambayo inaweza ikawa kubwa au kidogo, kwasababu…
soko la fedha linaathiriwa na maendeleo ya uchumi nchini na duniani.
Mifuko ya UTT
UTT ina mifuko 6;
✔ Mfuko wa Watoto
✔ Mfuko wa Ukwasi
✔ Mfuko wa Wekeza Maisha
✔ Mfuko wa Jikimu
✔ Mfuko wa Bond
✔ Mfumo wa Umoja
| Mfuko | Faida Yake | Unaweza Kutoa Fedha… | Kianzio (Shilingi) |
| Watoto | Kukuza Mtaji | Mpaka mtoto afike umri wa miaka 12 | 10,000/= |
| Ukwasi | Kukuza Mtaji | Ndani ya siku 3 za kazi | 100,000/= |
| Wekeza Maisha | Kukuza Mtaji | Baada ya miaka mitano (5) | 8,340/= kwa mwezi, au 1,000,000/= |
| Jikimu | Kutoa Gawio | Ndani ya siku 10 za kazi | 5,000/=Kwa ajili ya kukuza mtaji 1,000,000/=Kwa ajili ya gawio kila mwaka 2,000,000/=Kwa ajili ya gawio kila robo mwaka |
| Bond | Kutoa Gawio | Baada ya miezi 3-6 | 50,000/=Kwa ajili ya kukuza mtaji 5,000,000/=Kwa ajili ya gawio kila baada ya miezi 6 10,000,000/=Kwa ajili ya gawio kila mwezi |
| Umoja | Kukuza Mtaji | Ndani ya siku 10 za kazi | 10,000/= |
Tumia tracker kama ilivyoonyeshwa hapa chini kwa urahisi wa kufuatilia uwekezaji wako kila mwezi.

Usiache kufuatilia ukurasa wa Instagram kupata free content, na bofya kitufe hapo chini kuwasiliana nasi WhatsApp.
Hatujamalizana!
Kama una malengo ya kufikia kiwango fulani cha fedha ndani ya miaka kadhaa, unaweza ukafahamu utakachotakiwa kuweka kila mwezi kupitia:
PS:
Usisahau kwamba kila safari ndefu, ikiwemo uhuru wa kifedha, huanza na hatua moja, nayo ni hatua ya kwanza.
Anza leo!
Wako katika pesa,
Gracing Money!
Marejeo:
1] UTT-AMIS, uttamis.co.tz
2] UTT-AMIS, Investment Assumption Calculator, Monthly Investment Plan
Follow us on Socials

Read More Blog Posts
Umesikia Kuhusu Mifuko Sita (6) ya Uwekezaji ya iTrust?
Mifuko ya Uwekezaji ni mingi…na itazidi kuongezeka Je, umesikia kuhusu Mifuko ya Uwekezaji ya Pamoja… Imeongezeka na itaendelea kuongezeka. Kwa sasa ipo…
UTT ni nini?
UTT ni njia rahisi ya kuwekeza kwa watanzania. Elewa inavyofanya kazi na jinsi ya kuanza kuwekeza. Inawezekana umesikia kuhusu UTT lakini…
Jinsi ya Kuingia Kwenye Soko la Fedha BILA KWENDA KINYUME
Mwongozo wa Muislamu Kushiriki Soko la Fedha kwa Njia Halali na ya Kiimani Umesikia watu wanaongea kuhusu uwekezaji, kila kona ya…
Je, Wewe Kuwekeza Kwenye Kampuni la NICOL Utakua ni Uamuzi
Je, Wewe Kuwekeza Kwenye Kampuni la NICOL Utakua ni Uamuzi Sahihi? Kwenye picha hapo juu ni swali zuri nimeshawahi kuulizwa, na lilikua…
Jinsi ya Kuendesha Biashara Yako BILA KUPOTEZA UHURU Wako wa
Soma mpaka mwisho kama, una biashara ya kutoa huduma (service based business) au kuuza bidhaa (brick-and-mortar business), lakini unakabiliana na changamoto hizi; ✔…
VITABU VITANO Vinavyoweza KubadilishaMtazamo WAKO Kuhusu Pesa YAKO
Unataka kubadilisha mtazamo wa uchumi wako? Vitabu hivi vitano (5) vinaweza kubadilisha unavyofikiri kuhusu kipato, akiba na kukuza pesa yako. 6…
